sw_tn/gen/14/10.md

44 lines
1.6 KiB
Markdown
Raw Normal View History

2019-05-21 20:17:16 +00:00
# Sasa
Neno hili linatambulisha taarifa ya nyuma kuhusu bonde la Sidimu. Lugha yako inaweza kuwa na njia nyingine ya kutambulisha taarifa hii ya nyuma.
# lilikuwa limejaa mashimo ya lami
"ilikuwa na mashimo ya lami mengi". Haya yalikuwa mashimo katika ardhi ambayo yalikuwa na lami ndani mwao.
# lami
kimiminiko kinene, kinachonata, cheusi kinachotoka ardhini.
# wafalme wa Sodoma na Gomora
Huu ni usemi mwingine kwa ajili ya wafalme na majeshi yao. "wafalme wa Sodoma na Gomora na majeshi yao"
# wakaanguka pale
Maana zaweza kuwa 1) baadhi ya wanajeshi wao walianguka ndani ya mashimo ya lami au 2) wafalme wenyewe walianguka ndani ya mashimo ya lami. Kwa kuwa 14:17 unasema ya kwamba mfalme wa Sodoma alikwenda kukutana na Abramu, maana ya kwanza yaweza kuwa sahihi zaidi.
# Wale waliosalia
"Wale ambao hawakufa vitani na hawakuanguka ndani ya mashimo"
# adui
Hii ina maana ya mfalme Kedorlaoma na wafalme wengine na majeshi yao aliokuwa nao waliokuwa wakishambulia Sodoma na Gomora.
# mali zote za Sodoma na Gomora
Maneno "Sodoma" na "Gomora" ni lugha nyingine kwa ajili ya watu walioishi katika miji ile. "utajiri wa watu wa Sodoma na Gomora" au "mali za watu wa Sodoma na Gomora"
# vyakula vyao vyote
"chakula na vinywaji vyao"
# wakaenda zao
"wakaenda njia zao"
# wakamchukua pia Lutu, mtoto wa ndugu yake na Abramu ambaye aliishi Sodoma, pamoja na mali zake zote
Misemo ya "mwana wa kaka wa Abramu" na "aliyekuwa akiishi Sodoma" unamkumbusha msomaji juu ya mambo yaliyoandikwa mapema kuhus Lutu. "walimchukua Lutu pia, pamoja na na mali zake zote. Lutu alikuwa mwana wa kaka wa Abramu na alikuwa akiishi Sodoma kwa kipindi hicho"