sw_tn/psa/049/018.md

20 lines
945 B
Markdown
Raw Normal View History

2019-05-21 20:17:16 +00:00
# Akabariki nafsi yake
Hapa neno "nafsi" linamaanisha mtu mzima. Msemo huu unamaanisha kuwa alijiona kuwa na furaha na mafanikio kwa sababu ya utajiri wake. "Akajipongeza mwenyewe"
# na watu wanakusifu unapoishi kwa ajili yako mwenyewe
Hapa mwandishi anatoa kauli ya ujumla kuhusu jinsi watu wanavyozungumza kuhusu watu wengine waliofanikiwa kulingana na mtazamo wa kidunia.
# unapoishi kwa ajili yako mwenyewe
Msemo huu unamaanisha kuishi kwa mafanikio kulingana na mtazamo wa kidunia. "fanya vyema kwa ajili yako" au "ishi kwa mafanikio"
# ataenda katika kizazi cha baba zake
"ataenda mahali kizazi cha baba yake kilipo." Hii ni tasifida inayomaanisha kwamba mtu tajiri atakufa na kuungana na mababu zake kaburini. "ataungana na mababu zake kaburini"
# hawataona nuru tena
wale ambao "hawataona" ni mtu tajiri na mababu zake. Neno "nuru" inaweza kuwa inamaanisha jua au ni sitiari ya uhai. "hawataliona jua tena" au "hawataishi tena"