sw_tn/isa/03/10.md

36 lines
1.8 KiB
Markdown
Raw Permalink Normal View History

2019-05-21 20:17:16 +00:00
# Mwambie mtu mwenye haki ya kwamba itakuwa ni salama
"Mwambie yule ambaye anafanya kilicho haki ya kwamba nitafanya mambo kuwa mazuri kwake"
# mtu mwenye haki
Hii ina maana ya watu wenye haki kwa ujumla. "watu wenye haki"
# kwa maana watakula matunda ya matendo yao
Matendo yazungumziwa kana kwamba yalikuwa miti itoayo matunda yanayoweza kuliwa. Tunda ina maana ya dhawabu ya kufanya matendo mema. "kwa maana watapokea dhawabu yao kwa ajili ya matendo yao mazuri" au "kwa maana watapokea dhawabu yao kwa ajili ya mambo mazuri waliyofanya"
# watakula matunda ya matendo yao
Maandishi ya Kiebrania yana wingi wa kiwakilishi nomino hapa, lakini yana maana ya mtu mwenye haki yeyote. Watafsiri wanaweza kuchagua kutafsiri katika umoja. "atakula tunda la matendo yake"
# kwa maana fidia ya mikono yake itafanyika kwake
Hapa "mikono" ina maana ya matendo ambayo mtu amefanya. "kwa kile ambacho mtu mwovu amefanya kwa wengine itafanyika kwake"
# Watu wangu ... watu wangu
Maana zaweza kuwa 1) Isaya anazungumza na "wangu" kumaanisha Isaya, au 2) Yahwe anazungumza na "wangu" kumaanisha Yahwe.
# watoto ndio wakandamizaji wao
Maana zawvza kuwa 1) "watu wachanga wamekuwa viongozi wao na wanakandamiza watu" au 2) "viongozi wao hawajakomaa kama watoto na wanakandamiza watu"
# wanawake wanatawala juu yao
Maana zaweza kuwa 1) "wanawake wanatawala juu ya watu" au 2) "viongozi wao ni wadhaifu kama wanawake"
# wale wanaokuongoza wanakuongoza nje ya mstari na kuchanganya muelekeo wa njia yako
Ilikuwa kawaida katika Mashariki ya Kati ya Zamani kuzungumza juu ya viongozi wa taifa kana kwamba walikuwa wachungaji. Mchungaji huongoza kondoo katika njia nzuri katika usalama, viongozi wanapaswa kuwafunza watu ukweli na kuwasaidia kufanya kilicho sahihi. Viongozi wa Yuda hawakuwa wakifanya hivi. "viongozi wako ni kama wachungaji wabaya na hawakuonyeshi mahali pa kwenda"