sw_tn/gen/48/14.md

32 lines
1.3 KiB
Markdown
Raw Permalink Normal View History

2019-05-21 20:17:16 +00:00
# mkono wake wa kulia na kuuweka juu ya kichwa cha Efrahimu
Kuweka mkono wa kulia juu ya kichwa cha Efraimu ilikuwa ishara ya kwamba angepokea baraka kubwa.
# Israeli akambariki Yusufu
Hapa "Yusufu" pia ina maana ya Efraimu na Manase. Kwa kuwa Yusufu ni baba, ni yeye pekee anayetajwa hapa.
# Mungu ambaye mbele zake baba zangu Ibrahimu na Isaka walitembea
Kumtumikia Mungu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kutembea mbele za Mungu. "Mungu ambaye babu yangu Abrahamu na baba yangu Isaka alimtumikia"
# aliyenitunza
Mungu alimtunza Israeli kama vile mfugaji anavyotunza kondoo wake. "ambaye alinitunza kama mfugaji atunzavyo wanyama wake"
# malaika
Maana zinawezekana kuwa 1) hii ina maana ya malaika ambaye Mungu alimtuma kumlinda Yakobo au 2) hii ina maana ya Mungu aliyemtokea kama malaika kumlinda Yakobo.
# aliyenilinda
"aliniokoa"
# Jina langu na litajwe kwao, na majina ya baba zangu Abrahamu na Isaka
Hapa "jina" lina maana ya mtu mzima. Msemo "jina langu na litajwe kwao" ni lahaja ambayo ina maana ya kwamba mtu anakumbukwa kwa sababu ya mtu mwingine. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Watu wamkumbuke Abrahamu, Isaka, na mimi kwa sababu ya Efraimu na Manase"
# Na wawe makutano ya watu juu ya nchi
Hapa "wawe" ina maana ya Efraimu na Manase, lakini ina maana ya uzao wao. "Na wawe na uzao mwingi ambao utaishi ulimwenguni kote"